KISA CHA KIHISTORIA: KUANGUKA KWA UFALME WA MTEMI ISIKE TABORA, 1891
Mwaka 1891, Tabora ilikumbwa na tukio kubwa la kihistoria – vita kati ya Mtemi Isike, mtawala jasiri wa Unyanyembe, na wakoloni wa Kijerumani. Wajerumani walitaka kuchukua udhibiti wa eneo hilo, lakini Mtemi Isike alikataa katakata. Alijiandaa kwa vita akiwa na jeshi lake dogo, lakini lenye ari kubwa.
Baada ya mapambano makali na hatimaye kutishiwa kukamatwa, Mtemi Isike alichukua uamuzi mgumu. Badala ya kushuhudia adui akimvunjia heshima, aliamua kujiua kwa mlipuko wa baruti pamoja na familia yake katika ngome yake ya Itetemia.
Tukio hili lilimfanya Mtemi Isike kuwa miongoni mwa mashujaa wa kihistoria waliopinga ukoloni kwa gharama ya uhai wao.
Tags:
history