🏡 Kuhusu Kwetu

Kwetu ni taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) iliyozaliwa kutoka kiu ya mabadiliko na matumaini kwa vijana na jamii ya Mkoa wa Tabora. Tukiwa na kaulimbiu yetu “Elimika, Chukua Hatua”, tunajikita katika kuhamasisha, kuelimisha, na kuwezesha watu kuchukua hatua chanya kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na ya kijamii.-

📌 Malengo Yetu

Kutoa elimu kwa njia za ubunifu kupitia majarida, mitandao ya kijamii, na makongamano.

Kuibua na kusambaza hadithi za mafanikio ya vijana wa kawaida wanaofanya mambo makubwa.

Kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya kisasa kama nyenzo ya maendeleo kwa vijana.

Kuelimisha jamii juu ya afya bora, mazingira safi, na ustawi wa familia.

Kukuza ujasiriamali na kuunga mkono miradi ya vijana.

🌍 Maeneo Tunayogusa

✔️ Elimu na Maarifa

✔️ Afya na Mazingira

✔️ Ujasiriamali na Uchumi

✔️ Mahusiano na Malezi

✔️ Teknolojia na Ubunifu

✔️ Historia na Simulizi

✔️ Miradi na Mafanikio-

🧭 Dira Yetu

Kuwa jukwaa kuu la vijana na jamii kujifunza, kushirikishana, na kuchukua hatua za maendeleo endelevu.