🏡 Kuhusu Kwetu
Kwetu ni taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) iliyozaliwa kutoka kiu ya mabadiliko na matumaini kwa vijana na jamii ya Mkoa wa Tabora. Tukiwa na kaulimbiu yetu “Elimika, Chukua Hatua”, tunajikita katika kuhamasisha, kuelimisha, na kuwezesha watu kuchukua hatua chanya kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na ya kijamii.-
📌 Malengo Yetu
Kutoa elimu kwa njia za ubunifu kupitia majarida, mitandao ya kijamii, na makongamano.
Kuibua na kusambaza hadithi za mafanikio ya vijana wa kawaida wanaofanya mambo makubwa.
Kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya kisasa kama nyenzo ya maendeleo kwa vijana.
Kuelimisha jamii juu ya afya bora, mazingira safi, na ustawi wa familia.
Kukuza ujasiriamali na kuunga mkono miradi ya vijana.
---
🌍 Maeneo Tunayogusa
✔️ Elimu na Maarifa
✔️ Afya na Mazingira
✔️ Ujasiriamali na Uchumi
✔️ Mahusiano na Malezi
✔️ Teknolojia na Ubunifu
✔️ Historia na Simulizi
✔️ Miradi na Mafanikio-
--
🧭 Dira Yetu
Kuwa jukwaa kuu la vijana na jamii kujifunza, kushirikishana, na kuchukua hatua za maendeleo endelevu.
---
🤝 Tunachofanya
Tunakusanya simulizi za maisha halisi kutoka kwa vijana mashujaa wa Tabora na Tanzania kwa ujumla.
Tunatengeneza content zenye tija na kuelimisha kupitia mitandao, video, na machapisho.
Tunaandaa kampeni, mashindano, na michezo ya kidigitali kama njia ya kuwahamasisha vijana kushiriki.
---
📲 Tuungane
Tovuti Yetu: www.kwetu.online
Facebook | Instagram | TikTok | X: @Kwetu
WhatsApp: +255 xxxxxx
---
🟢 Kwetu siyo tu jina – ni mwamko wa kizazi kipya cha mabadiliko.