KWETU

Kwetu ni taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) inayojikita katika kuhamasisha na kuwezesha jamii, hususan vijana wa Mkoa wa Tabora, kupitia elimu, afya, ujasiriamali, mazingira, na matumizi ya teknolojia ya kisasa. Tunakusanya na kusambaza hadithi za mafanikio, tunaandaa majarida ya kuelimisha, na tunahamasisha jamii kuchukua hatua chanya kwa maendeleo endelevu. Kupitia kaulimbiu yetu “Elimika, Chukua Hatua,” tunaamini kila mtu ana nafasi ya kuleta mabadiliko kwenye jamii yake.
Tovuti yetu: www.kwetu.online

CHANGAMOTO YA MSONGO WA MAWAZO YAMPOTEZA KIJANA DOTTO CHACHA – KILOLENI, TABORA

CHANGAMOTO YA MSONGO WA MAWAZO YAMPOTEZA KIJANA DOTTO CHACHA – KILOLENI, TABORA
Katika siku za hivi karibuni, tumepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya msiba mzito uliotokea Kiloleni, Manispaa ya Tabora – ambapo kijana mwenzetu Dotto Chacha alipoteza maisha kwa kujinyonga kutokana na msongo wa mawazo.

🖤 Tukio hili limetuacha na majonzi, lakini pia linatufungua macho juu ya uhalisia wa changamoto za afya ya akili, hususani kwa vijana.

✳️ Dotto alikuwa nani?

Dotto Chacha alikuwa kijana mchapakazi, mwenye ndoto na matumaini. Lakini kwa bahati mbaya msongo wa mawazo kutokana na kupata majeraha mbali mbali sehemu ya mwili wake baada ya kupata ajari. Kumpelekea kufanya maamuzi magumu na yakuhudhunisha. 

---

🟢 Kwetu, tunasimamia haya:

✅ Kuhamasisha jamii kusikiliza zaidi kuliko kulaumu
✅ Kujenga utamaduni wa mazungumzo ya wazi kuhusu afya ya akili
✅ Kuelimisha mashuleni, mitaani na kwenye majukwaa ya kidijitali kuhusu namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo
✅ Kutoa nafasi kwa vijana kupata msaada wa kitaalamu au wa karibu kupitia kampeni zetu

---

🕊️ Tunatoa pole nyingi

Kwa familia ya Dotto, marafiki, jirani na jamii yote ya Kiloleni – tupo pamoja nanyi.
Tukio hili liwe mwanga mpya wa sisi kama jamii kuona, kuelewa, na kusaidia kabla ya kuhukumu.

🟢 Kama una changamoto yoyote ya kisaikolojia au unajisikia kupotea, tafadhali zungumza na mtu, tafuta msaada. Upo kwa thamani. Tupo kwa ajili yako.

---

ELIMIKA. CHUKUA HATUA.
KWETU – Tabora. Tanzania.
Previous Post Next Post